Moja kwa moja, Mbunge wa Marekani: Trump na washirika wake wamenufaika na vita dhidi ya Iran

Hakuna ushahidi unaothibitisha moja kwa moja madai ya Warren kuhusu uhusiano kati ya michango ya kampeni na faida zinazodaiwa kupatikana kutokana na vita hivyo.

Muhtasari

Ruka Video uendelee
  • xx
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Kiongozi wa upinzani nchini Zambia ashtakiwa kwa uhaini

    Brian Mundubile

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Kiongozi wa upinzani nchini Zambia, Brian Mundubile, ameshtakiwa kwa uhaini, kwa mujibu wa wakili wake, katika hatua inayokuja wakati wa mvutano wa kisiasa kufuatia uchaguzi wa urais uliopita.

    Mundubile alikamatwa Alhamisi baada ya operesheni ya usalama iliyomlazimu kujificha kwa muda. Mwanasiasa huyo alikuwa amepinga matokeo ya uchaguzi uliompa Rais Hakainde Hichilema ushindi wa muhula wa pili.

    Mamlaka zilidai kuwa chama cha Mundubile, NRPUP, kilikuwa kinapanga uasi wa kutumia silaha, madai ambayo chama hicho kimeyakanusha.

    Akizungumza Jumamosi usiku, wakili wake Milner Katolo alisema mteja wake atafikishwa mahakamani kujibu shtaka la uhaini. Aliongeza kuwa watu wengine 17, wakiwemo mgombea mwenza wa Mundubile, Makebi Zulu, pia wanakabiliwa na mashtaka hayo.

    Kwa mujibu wa matokeo rasmi, Mundubile alipata asilimia 38 ya kura katika uchaguzi wa Agosti 13, huku Hichilema akishinda kwa asilimia 60.

    Siku moja baada ya uchaguzi, vikosi vya usalama vilivamia jengo lililohusishwa na kiongozi huyo wa upinzani mjini Lusaka. Operesheni hiyo iliripotiwa kusababisha kifo cha waziri wa zamani na kuwakamata wanasiasa kadhaa.

    Baadaye Mundubile na Zulu walikimbilia katika jengo la Umoja wa Mataifa mjini Lusaka kabla ya kutiwa mbaroni na mamlaka za Zambia.

    Wakati huo huo, upinzani unasema haukuweza kuwasilisha pingamizi mahakamani dhidi ya matokeo ya uchaguzi kwa sababu mahakama zilikuwa zimefungwa siku ya mwisho wa muda wa kisheria wa kufungua kesi.

    Rais Hichilema anatarajiwa kuapishwa kwa muhula wake wa pili tarehe 1 Septemba.

    Waangalizi wa uchaguzi walisema upigaji kura ulikuwa wa amani kwa kiasi kikubwa, ingawa Tume ya Haki za Kibinadamu ya Zambia imetoa wito wa uchunguzi kuhusu watu wanaodaiwa kutoweka baada ya operesheni za usalama zilizofanyika wakati wa uchaguzi.

  2. Messi afunga mabao manne Inter Miami ikiifunga Montreal 7-1

    Lionel Messi amefikisha mabao 18 katika msimu huu wa Ligi Kuu ya Marekani (MLS).

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Lionel Messi amefunga mabao manne na kutoa pasi moja ya bao huku Inter Miami ikiichapa Montreal mabao 7-1 katika mechi ya Major League Soccer (MLS), na kurejea kwenye njia ya ushindi baada ya kipindi kigumu cha matokeo.

    Nyota huyo wa Argentina mwenye umri wa miaka 39 aliifungia Miami mabao manne, likiwemo bao la mpira wa adhabu na hat-trick yake katika kipindi cha pili, huku pia akimsaidia Luis Suarez kufunga.

    Ushindi huo ulikuwa wa kwanza kwa Miami baada ya kushinda mechi moja pekee katika michezo saba tangu kurejea kwa Messi kutoka Kombe la Dunia la Klabu mapema mwezi huu.

    Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Messi kufunga mabao manne katika mechi ya MLS na kumfikisha mabao 18 msimu huu, hivyo kuwa kinara wa ufungaji wa ligi hiyo.

    Kocha wa muda wa Inter Miami, Guillermo Hoyos, alimsifu Messi akisema: “Hakuna maneno ya kuelezea uzuri wa soka kama huo.”

  3. Baadhi ya safari za ndege nchini Kenya zacheleweshwa - Kunani?

    Wasafiri katika Uwanja wa Kimataifa wa JKIA

    Chanzo cha picha, Reuters

    Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Kenya (KAA) imetangaza kuwa baadhi ya ndege zinazoondoka katika viwanja vya ndege nchini humo zitachelewa.

    Kupitia taarifa iliyotolewa Jumapili, KAA imesema inashirikiana kwa karibu na mashirika ya usafiri wa anga, kampuni za ndege na wadau wengine katika sekta hiyo ili kudhibiti hali hiyo, kupunguza usumbufu kwa wasafiri na kuhakikisha shughuli za viwanja vya ndege zinaendelea kwa ufanisi.

    Mamlaka hiyo imewashauri abiria kuwasiliana na kampuni zao za ndege ili kupata taarifa za hivi karibuni kuhusu ratiba za safari zao na kupanga safari zao ipasavyo.

    KAA pia imeomba radhi kwa usumbufu unaotokana na ucheleweshaji huo na kuwashukuru abiria kwa uvumilivu wao wakati juhudi za kurejesha hali ya kawaida zikiendelea.

    Mamlaka hiyo imesema itaendelea kutoa taarifa zaidi kadri hali itakavyoendelea kubadilika.

  4. Netanyahu alaani vurugu za walowezi Ukingo wa Magharibi

    Netanyahu

    Chanzo cha picha, Reuters

    Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amelaani mashambulizi yaliyofanywa na walowezi wa Israel dhidi ya vijiji vya Wapalestina vya Qusra na Jalud katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.katika tukio la hivi punde la mivutano ambayo imedumu kwa karibu wiki tatu.

    Katika hatua isiyo ya kawaida, Netanyahu alilaani kile alichokiita "vitendo vya uhalifu na vurugu" vilivyofanyika katika vijiji viwili vya Wapalestina siku ya Jumamosi. Aliwataja walowezi hao kama "kundi dogo la wahuni wasioheshimu sheria."

    Katika taarifa, alisema, "Ninelaani vikali vitendo vya uhalifu na vurugu vilivyofanywa katika vijiji vya Qusra na Jalud na wahuni wachache wasioheshimu sheria; watu ambao wanaitendea dhuluma kubwa jamii ya Wayahudi wanaoheshimu sheria, wanazuia kazi ya jeshi la Israel katika kutekeleza majukumu yake, na kuharibu taswira ya Israel katika nyanja ya kimataifa."

    Rais wa Israel Isaac Herzog alilaani vurugu hizo, akizielezea kama "uvukaji wa mstari mwekundu uliofanywa na watu wanaokiuka sheria, ambao wanatenda kinyume kabisa na sheria na maadili ya Taifa la Israel," na kusema kuwa kilichotokea ni "doa kwa sifa ya Israel."

    Wakazi wa Qusra na jeshi la Israel walisema kuwa makumi ya walowezi walivamia kijiji hicho, wakawarushia mawe wakazi na kuwalazimisha baadhi yao kujifungia majumbani mwao.

    Ripoti zaidi zinasema walowezi wa Israel waliovaa barakoa waliwashambulia na kuwajeruhi wafanyakazi wa NBC News pamoja na mwanamke Mpalestina katika kijiji cha Jalud, karibu na Qusra, katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa.

    Wakati huo huo, raia mmoja Mpalestina mwenye uraia wa Marekani alikuwa akielekea Qusra akisema anataka kufika kwa familia yake iliyokuwa imezingirwa na walowezi.

    Jeshi la Israel limesema lilituma wanajeshi na polisi wa mpakani eneo hilo baada ya kupokea taarifa za makabiliano kati ya waandamanaji wa Israel na Wapalestina, yaliyojumuisha kurushiana mawe.

    Soma pia:

  5. Kim Jong Un amfuta kazi Waziri wake wa Ulinzi

    Gwaride la jeshi la Korea Kaskazini

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, amemfuta kazi Waziri wa Ulinzi na kufanya mabadiliko kadhaa katika ngazi za juu za jeshi, kulingana na vyombo vya habari vya serikali.

    Shirika la habari la KCNA limesema uamuzi huo ulifikiwa katika mkutano ulioongozwa na Kim Jong Un, ambapo viongozi walijadili kile kilichoelezwa kuwa mpango wa marekebisho ya muundo wa jeshi.

    Kwa mujibu wa KCNA, Noh Kwang-chul ameondolewa katika wadhifa wa Waziri wa Ulinzi na kushushwa cheo kuwa naibu mkuu wa kwanza wa Idara ya Viwanda vya Silaha ndani ya chama tawala.

    Nafasi hiyo sasa itashikiliwa na Kim Song-gi, ambaye alikuwa mkuu wa Idara Kuu ya Siasa ya Jeshi la Watu wa Korea.

    Katika mabadiliko hayo, mshauri wa masuala ya ulinzi wa Kim Jong Un, Pak Jong-chun, ameteuliwa kuwa makamu mwenyekiti wa Tume Kuu ya Kijeshi pamoja na kuwa mjumbe wa Politburo ya Chama cha Wafanyakazi wa Korea.

    Vyombo vya habari vya serikali havikutoa sababu za mabadiliko hayo. Hata hivyo, hatua hiyo imekuja wakati Korea Kaskazini ikiendelea kuimarisha uwezo wake wa kijeshi na kuimarisha ushirikiano wa kiulinzi na Urusi, huku mvutano katika Rasi ya Korea ukiendelea.

    Pia unaweza kusoma:

  6. Tishio dhidi ya mwana wa Netanyahu lasababisha kuondolewa kwake Marekani - ripoti

    Netanyahu

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Vyombo kadhaa vya habari vya Israel vimeripoti kuwa shirika la usalama wa ndani la nchi hiyo, Shin Bet, limethibitisha kile lilichokitaja kuwa tishio kubwa dhidi ya Yair Netanyahu, mwana wa Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu.

    Kwa mujibu wa ripoti hizo, tathmini ya usalama ilisababisha uamuzi wa kumhamisha Yair Netanyahu kutoka Marekani kwenda Israel pamoja na kikosi chake cha ulinzi.

    Taarifa hizo zimekuja baada ya kuibuka kwa ripoti kuhusu safari yake ya dharura kutoka Florida kwenda Israel. Shin Bet haijatoa maelezo zaidi kuhusu asili ya tishio lililoripotiwa au waliotuhumiwa kuhusika.

    Hivi karibuni, Benjamin Netanyahu alidai kuwa Iran ilikuwa imejaribu kumuua mmoja wa wanawe, ingawa hakumtaja kwa jina wakati huo. Ripoti za sasa zinaeleza kuwa alikuwa akimuashiria Yair Netanyahu.

    Kwa upande wake, Iran imewahi kukanusha madai ya kuhusika katika njama za mauaji dhidi ya viongozi au watu mashuhuri wa kisiasa wa Marekani na Israel.

    Kufikia sasa, Tehran haijatoa tamko rasmi kuhusu taarifa hiyo ilizoripotiwa na vyombo vya habari vya Israel.

    Maelezo zaidi:

  7. Mbunge wa Marekani: Trump na washirika wake wamenufaika na vita dhidi ya Iran

    Donald Trump

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Rais wa Marekani Donald Trump

    Seneta wa chama cha Democratic, Elizabeth Warren, amemtaja Donald Trump kuwa "rais fisadi zaidi katika historia ya Marekani" wakati akimkosoa kuhusu sera zake kuhusiana na Iran na sekta ya mafuta.

    Akizungumza katika mkutano wa kampeni, Warren alidai kuwa baadhi ya makampuni makubwa ya mafuta yaliyounga mkono kampeni ya Trump yamenufaika pakubwa kutokana na vita dhidi ya Iran.

    "Donald Trump anapoanzisha vita na Iran na marafiki zake wa sekta ya mafuta, ambao walichangia kampeni yake, wakipata faida kubwa kutokana na vita hivi, ni wajibu wetu kufichua hali hiyo na kuipinga," alisema Warren.

    Warren hakutaja kampuni yoyote mahsusi kuhusiana na madai hayo. Wakati huo huo, ongezeko la bei ya mafuta na faida kubwa zilizoripotiwa katika baadhi ya kampuni za sekta ya nishati limekuwa likifuatiliwa kwa karibu na wachambuzi katika miezi ya hivi karibuni.

    Hata hivyo, hakuna ushahidi uliowasilishwa unaothibitisha moja kwa moja madai ya Warren kuhusu uhusiano kati ya michango ya kampeni na faida zinazodaiwa kupatikana kutokana na vita hivyo.

    Kwa upande wake, Trump amewahi kukosoa kupanda kwa bei ya mafuta na kuwataka wazalishaji kuongeza uzalishaji ili kusaidia kudhibiti bei.

    Soama zaidi:

  8. Natumai hujambo. Karibu kwa matangazo ya moja kwa moja.